SURA YA 95 SHERIA YA MADAWA NA UZUIAJI WA USAFIRISHAJI WA MADAWA HARAMU SHERIA KUU MPANGILIO WA VIFUNGU SEHEMU YA 1 MASHARTI YA MWANZO

Σχετικά έγγραφα
IDARA YA UTUMISHI WA MWALIMU

MUONGOZO RAHISI WA RAIA KUHUSU UCHAGUZI KATIKA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA MWAKA 2014

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII

KILIMO CHA ZAO LA VANILLA

Mradi wa Misitu ya Jamii MJUMITA (Lindi) Wilaya ya Lindi Vijijini na Manispaa ya Lindi, Mkoa wa Lindi, Tanzania

Kuondoa Utata Uliyomo katika Tafauti ya Muandamo

i Kiswahili (TE) Class 1.indd i 5/30/14 8:07 PM


Yaliyomo. ~ Ukurasa 3 ~

Hadiyth Ya 11 Daraja Za Iymaan Ni Sabini Na Kitu; Ya Juu Ni Tawhiyd, Na Ya Chini Kabisa Ni Kuondosha Taka Njiani


IMAM MAHDI (A.S.) NI TUMAINI LA MATAIFA

Kiswahili TE(C2).indd i 5/30/14 8:14 PM

Hadiyth Ya 61 Dunia Ni Kama Kivuli Anachokitumia Msafiri Kwa Muda Tu

Hadiyth Ya 71 Jikinge Na Moto Japo Kwa Tende Au Neno Jema )) :

Hadiyth Ya 131 Allaah Ameridhia Kuabudiwa, Kutokumshirikisha, Kuungana Na Anachukia Uvumi, Udadisi Na Kupoteza Mali ( )

Mafundisho Ya Madhehebu

AHLUL ~ KISAA. Mkusanyiko wa sifa na tarehe za Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), Imamu Ali, Bibi Fatimah, Imamu Hassan na Imamu Hussein

Idghaam haiwezekani ikawa katika neno moja bali ni lazima nuwn saakinah au tanwiyn iweko mwisho wa neno la kwanza, na herufi inayoingizwa hiyo

Hadiyth Ya 1 Allaah Hatazami Miili Wala Sura, Bali Anatazama Nyoyoni

Hadiyth Ya 111 Wanaume Na Wanawake Wasio Maharimu Wasitazamane Uchi Wala Wasilale Pamoja

MATESO YA DHURIA YA MTUME

Ni kusimama katika neno lakini hata ukiunganisha yanayofuatia haiharibu maana. Ni lazima kusimama kwani kuunganisha na yanayofuatia kutaharibu maana.

Ummu Iyyaad Imepitiwa Na: Abu Abdillaah Muhammad Baawazir

25-Faharasa. Matamshi. Tamshi moja ni lafdhw. Iliyo na nguvu kabisa, inayodhaniwa kuwa sahihi kabisa, rai inayokubalika kabisa.

ΛΕΞΙΚΟΝ ΕΛΛΗΝΟ-ΣΟΥΑΧΙΛΙ

05- Fadhila Za Umrah Na Hajj

2742/ 207/ / «&»

Ni hamzah inayotamkwa katika neno na haitamkwi (hutoweka) wakati wa kuunganisha na neno la nyuma yake.

( ) 1995.» 3 ( ). 10 ( ) ( ) 1986, ( ) (1) 3,, ( ),,,,».,,,

ί α α I. Β α μ α π α μ α μ π φα α υ α υ αμ α ία ( α. μ3) : ία & α μα μα - αμ υ α ) α α Θ π μα α 79 (55) * 107

,+ 2 1ntr0du~a0 TABLE OF CONTENTS. a * 4. LT\,? .fi T? PAGE. n - q;.;.+e Afos ao carbono. Conepxakiue. CTpa~uqa ~Zgina Ukuras a

Νόµοςπεριοδικότητας του Moseley:Η χηµική συµπεριφορά (οι ιδιότητες) των στοιχείων είναι περιοδική συνάρτηση του ατοµικού τους αριθµού.

A. Αὐτοτελεῖς δημοσιεύσεις:

Estimation of grain boundary segregation enthalpy and its role in stable nanocrystalline alloy design

ΠΡΟΣΚΛΗΣΗ ΕΚΔΗΛΩΣΗΣ ΕΝΔΙΑΦΕΡΟΝΤΟΣ

ΝΟΜΟΣ ΤΗΣ ΠΕΡΙΟ ΙΚΟΤΗΤΑΣ : Οι ιδιότητες των χηµικών στοιχείων είναι περιοδική συνάρτηση του ατοµικού τους αριθµού.

, &

K r i t i k i P u b l i s h i n g - d r a f t

Ispitivanje toka i skiciranje grafika funkcija

ΓΗ ΚΑΙ ΣΥΜΠΑΝ. Εικόνα 1. Φωτογραφία του γαλαξία μας (από αρχείο της NASA)

ΤΓΓΡΑΜΜΑ 1: (HUGH D. YOUNG, 8 Ζ ΔΚΓΟΖ, ΔΚΓΟΔΗ ΠΑΠΑΕΖΖ)

ΕΙΣΑΓΩΓΗ ΣΤHN. Δρ. Α. ΤΖΑΝΗ

ΕΛΤΙΟ ΤΥΠΟΥ. ΕΙΚΤΗΣ ΤΙΜΩΝ ΥΛΙΚΩΝ ΚΑΤΑΣΚΕΥΗΣ ΝΕΩΝ ΚΤΙΡΙΩΝ ΚΑΤΟΙΚΙΩΝ: εκέµβριος 2015 (2010=100,0)

ΚΑΤΑΣΤΑΤΙΚΟΣ ΧΑΡΤΗΣ ΑΡΧΩΝ ΕΝΑΝΤΙ ΤΩΝ ΠΟΛΙΤΩΝ ΣΤΗΝ «ΚΟΙΝΩΝΙΑ ΤΗΣ ΓΝΩΣΗΣ» ΕΙΣΗΓΗΤΗΣ:ΜΟΧΙΑΝΑΚΗΣ ΚΩΣΤΗΣ ΠΡΟΪΣΤΑΜΕΝΟΣ ΠΛΗΡΟΦΟΡΙΚΗΣ ΔΗΜΟΥ ΗΡΑΚΛΕΙΟΥ

ΟΙ ΜΙΚΡΟΜΕΣΑΙΕΣ ΕΠΙΧΕΙΡΗΣΕΙΣ ΣΤΗΝ ΕΛΛΑΔΑ ΚΑΙ Ο ΚΛΑΔΟΣ ΤΗΣ ΥΠΟΔΗΣΗΣ

ΚΑΝΟΝΙΣΜΟΣ (EE) 2019/1238 ΤΟΥ ΕΥΡΩΠΑΪΚΟΥ ΚΟΙΝΟΒΟΥΛΙΟΥ ΚΑΙ ΤΟΥ ΣΥΜΒΟΥΛΙΟΥ

bab.la Φράσεις: Ταξίδι Τρώγοντας έξω ελληνικά-ελληνικά

..,..,.. ! " # $ % #! & %

Language, Mobile Phones and Internet: A Study of SMS Texting, , IM and SNS Chats in Computer Mediated Communication (CMC) in Kenya

15/01/2015 Αναλυτικό Πρόγραµµα Σπουδών 09:07:38

Για να εμφανιστούν σωστά οι χαρακτήρες της Γραμμικής Β, πρέπει να κάνετε download και install τα fonts της Linear B που υπάρχουν στο τμήμα Downloads.

ΕΞΕΤΑΣΤΙΚΗ ΠΕΡΙΟΔΟΣ ΦΕΒΡΟΥΑΡΙΟΥ 2011 ΟΙΚΟΝΟΜΙΚΑ ΚΑΙ ΧΡΗΜΑΤΟΟΙΚΟΝΟΜΙΚΑ ΜΑΘΗΜΑΤΙΚΑ 14 ΦΕΒΡΟΥΑΡΙΟΥ 2011

ΙΑΦΑ Φ ΝΕΙ Ε ΕΣ Ε ΧΗΜΕ Μ Ι Ε ΑΣ ΓΥΜΝ Μ ΑΣΙΟΥ H

(5), (8) (9), (10) (11),

Å/ ÅÃ... YD/ kod

1.7 ΟΡΙΟ ΣΥΝΑΡΤΗΣΗΣ ΣΤΟ ΑΠΕΙΡΟ

Ovo nam govori da funkcija nije ni parna ni neparna, odnosno da nije simetrična ni u odnosu na y osu ni u odnosu na

ΑΞΙΟΛΟΓΗΣΗ ΤΗΣ ΕΡΓΟΛΑΒΙΚΗΣ ΚΑΤΟΙΚΙΑΣ ΩΣ ΕΠΕΝΔΥΣΗ

ΠΟΣΟΤΙΚΕΣ ΜΕΘΟΔΟΙ ΔΕΟ 13 ΤΟΜΟΣ Δ ΣΤΑΤΙΣΤΙΚΗ ΓΙΑ ΤΗ ΔΙΟΙΚΗΣΗ ΕΠΙΧΕΙΡΗΣΕΩΝ

ΠΕΡΙΕΧΟΜΕΝΑ ΠΡΟΛΟΓΟΣ Ι - ΔΙΟΙΚΗΣΗ, ΓΡΑΜΜΑΤΕΙΑ... 13

APPENDIX I PITTSBURGH NO. 8 WASHABILITY DATA AND RECOVERY- CURVES

ZBIRKA POTPUNO RIJEŠENIH ZADATAKA

Α Π Ο Φ Α Σ Η 4/459/ του ιοικητικού Συµβουλίου

Αριθμός αποφάσεως 5928/2010 ΤΟ ΠΟΛΥΜΕΛΕΣ ΠΡΩΤΟΔΙΚΕΙΟ ΠΕΙΡΑΙΑ (Διαδικασία Εκούσιας Δικαιοδοσίας)

ΗΜΟΣΙΕΥΕΙ ΕΙ ΟΠΟΙΗΣΗ ΣΤΟΝ ΙΚΤΥΑΚΟ ΤΟΠΟ ΤΟΥ ΧΡΗΜΑΤΙΣΤΗΡΙΟΥ ΤΟΥ ΛΟΥΞΕΜΒΟΥΡΓΟΥ

Η ΔΙΔΑΣΚΑΛΙΑ ΤΗΣ ΘΡΗΣΚΕΙΑΣ ΣΤΟ ΟΥΔΕΤΕΡΟΘΡΗΣΚΟ ΣΧΟΛΕΙΟ (ΤΟΥ ΡΕΖΙΣ ΝΤΕΜΠΡΕ)

Για κάθε διδακτική ενότητα ακολουθείται η λεγόμενη τετραμερής πορεία, χωρίζεται δηλαδή η διδασκαλία σε τέσσερα κύρια στάδια.

ΔΕΛΤΙΟ ΜΗΝΙΑΙΩΝ ΣΤΟΙΧΕΙΩΝ ΓΕΝΙΚΗΣ ΚΥΒΕΡΝΗΣΗΣ ΝΟΕΜΒΡΙΟΣ 2014

ΕΛΛΗΝΙΚΗ ΔΗΜΟΚΡΑΤΙΑ. 18:00-20:00 Π. αμφ, 002, 201, 202, 203, ΔΕΧΡΗ16-ΔΙΑΧΕΙΡΙΣΗ ΚΙΝΔΥΝΟΥ Α - Ω ΔΕΧΡΗ16

Συμβούλιο της Ευρωπαϊκής Ένωσης Βρυξέλλες, 7 Μαρτίου 2017 (OR. en)

Meren virsi Eino Leino

ΔΙΕΡΕΥΝΗΣΗ ΛΕΙΤΟΥΡΓΙΑΣ ΟΡΓΑΝΩΜΕΝΩΝ ΧΩΡΩΝ ΣΤΑΘΜΕΥΣΗΣ ΔΙΚΥΚΛΩΝ ΣΤΟ ΚΕΝΤΡΟ ΤΗΣ ΘΕΣΣΑΛΟΝΙΚΗΣ

Institutional Repository - Library & Information Centre - University of Thessaly 01/02/ :17:35 EET

Μοντελοποίηση Στατικού Ηλεκτρισμού Νικόλας Νικολάου Καθηγητής φυσικής Λύκειο Αγίου Αντωνίου

Γίτσα Σοντζόγλου-Κοτταρίδη. Η ΤΡΙΤΗ ΗΛΙΚΙΑ: ΜΥΘΟΣ ΚΑΙ ΠΡΑΓΜΑΤΙΚΟΤΗΤΑ** Σκέψεις για μια επιστημονική έρευνα

ΣΧΟΛΗ ΕΠΙΣΤΗΜΩΝ ΙΟΙΚΗΣΗΣ ΕΠΙΧΕΙΡΗΣΕΩΝ ΤΜΗΜΑ ΛΟΓΙΣΤΙΚΗΣ ΚΑΙ ΧΡΗΜΑΤΟΟΙΚΟΝΟΜΙΚΗΣ

Κεφάλαιο 5 Όριο και συνέχεια συνάρτησης

Si + Al Mg Fe + Mn +Ni Ca rim Ca p.f.u

ΔΕΛΤΙΟ ΜΗΝΙΑΙΩΝ ΣΤΟΙΧΕΙΩΝ ΓΕΝΙΚΗΣ ΚΥΒΕΡΝΗΣΗΣ ΙΟΥΛΙΟΣ 2014

(2), ,. 1).

ΑΣΚΗΣΕΙΣ ΣΤΙΣ ΕΞΙΣΩΣΕΙΣ

Στρωματογραφία-Ιστορική γεωλογία. Κρυπτοζωικός Μεγααιώνας Δρ. Ηλιόπουλος Γεώργιος Σχολή Θετικών Επιστημών Τμήμα Γεωλογίας

COURBES EN POLAIRE. I - Définition

ΣΔΥΝΟΛΟΓΗΚΟ ΠΑΝΔΠΗΣΖΜΗΟ ΚΤΠΡΟΤ ΥΟΛΖ ΜΖΥΑΝΗΚΖ ΚΑΗ ΣΔΥΝΟΛΟΓΗΑ ΠΣΤΥΗΑΚΖ ΔΡΓΑΗΑ:

ΠΟΡΙΣΜΑ ΠΡΟΣ ΕΝΑ ΝΕΟ ΚΟΙΝΩΝΙΚΟ ΣΥΜΒΟΛΑΙΟ ΓΙΑ ΤΙΣ ΣΥΝΤΑΞΕΙΣ

Αλληλεπίδραση ακτίνων-χ με την ύλη

Εβδομαδιαία έκθεση επιδημιολογικής επιτήρησης της λοίμωξης από ιό του Δυτικού Νείλου σε ανθρώπους, Ελλάδα, 14 Αυγούστου 2013

Διαχρονικές Τάσεις Δεικτών Ανθρώπινου Δυναμικού στην Κύπρο: Συμμετοχή και Προσφορά στην Αγορά Εργασίας

ΚΑΝΟΝΙΣΜΟΣ (ΕΕ) 2019/1243 ΤΟΥ ΕΥΡΩΠΑΪΚΟΥ ΚΟΙΝΟΒΟΥΛΙΟΥ ΚΑΙ ΤΟΥ ΣΥΜΒΟΥΛΙΟΥ

στο σχέδιο νόµου «Κύρωση του Πρωτοκόλλου µεταξύ το οποίο τροποποιεί τη Σύµβαση µεταξύ της Ελληνικής Δηµοκρατίας και της Ελβετικής Συνοµοσπονδίας

ΜΑΘΗΜΑ ΠΕΜΠΤΟ ΤΥΠΟΛΟΓΙΑ ΚΑΙ ΛΕΞΙΛΟΓΙΟ

3. α) = + 13 β) = + 10 γ) = + 9 δ) = = 0-3 = - 2 = - 1 = = + 1 = + 2 =

Το άτομο του Υδρογόνου

lujo οό ΚΕΦΑΛΑΙΟ A Κυριότητα ακινήτου /. Γενικά 2. Κυριότψα βεβεφημένη με περιορισμένα εμπράγματα δικαιώματα 3. Μετακλητή κυριότψα

ΚΕΝΤΡΙΚΗ ΕΠΙΤΡΟΠΗ ΕΙΔΙΚΩΝ ΜΑΘΗΜΑΤΩΝ ΣΑΒΒΑΤΟ 28 ΙΟΥΝΙΟΥ 2003 ΕΞΕΤΑΖΟΜΕΝΟ ΜΑΘΗΜΑ: ΕΛΕΓΧΟΣ ΜΟΥΣΙΚΩΝ ΑΚΟΥΣΤΙΚΩΝ ΙΚΑΝΟΤΗΤΩΝ

Λίζα Βάρβογλη Εικονογράφηση: Γιώργος Πετρίδης

ΗΜΔΙΩΔΙ ΑΣΙΚΟΤ ΓΙΚΑΙΟΤ (ΜΔΡΟ Γ )

ΠΡΑΞΗ ΔΙΟΙΚΗΤΗ ΑΡΙΘΜ. 2590/ ΘΕΜΑ: Ελάχιστες Κεφαλαιακές Απαιτήσεις των Πιστωτικών Ιδρυμάτων για το Λειτουργικό Κίνδυνο

Αριθμός 3121/2014 ΤΟ ΠΟΛΥΜΕΛΕΣ ΠΡΩΤΟ ΙΚΕΙΟ ΠΕΙΡΑΙΩΣ ( ιαδικασία Εκουσίας ικαιοδοσίας)

Transcript:

SURA YA 95 SHERIA YA MADAWA NA UZUIAJI WA USAFIRISHAJI WA MADAWA HARAMU SHERIA KUU MPANGILIO WA VIFUNGU SEHEMU YA 1 MASHARTI YA MWANZO Kifungu Jina 1. Jina fupi na matumizi 2. Tafsiri SEHEMU YA II KUUNDWA KWA TUME YA WIZARA ZINAZOTEGEMEANA YA KURATIBU UDHIBITI WA MADAWA 3. Wajibu wa Serikali katika kuzuia matumizi mabaya ya dawa. 4. Kuundwa kwa Tume kitaifa ya kuratibu madawa. 5. Kazi za Tume. 6. Ripoti za Tume kupelekwa Bungeni 7. Bajeti ya Tume 8. Kamishna kushiriki katika mikutano ya wizara zinazotegemeana. 9. Kamishna kuandaa maamuzi na kuhakikisha utekelezaji. 10. Tume kutumia fedha kwa matumizi mbalimbali. SEHEMU YA TATU MFUKO WA UDHIBITI WA MATUMIZI MABAYA YA MADAWA 11. Kuanzishwa kwa Mfuko SEHEMU YA IV UZUIAJI WA UMILIKI NA USAFIRISHAJI WA DAWA NA VITU VYA KULEVYA NA KULIMA WA MAZAO FULANI 12. Uzuiaji wa kilimo cha mimea na vitu fulani. 13. Uwezo wa Tume kuruhusu, kudhibiti na ulimaji, uzalishaji au uuzaji n.k wa afyuni,majani ya koka,n.k. 1

14. Madawa ya kulevya hayatashikiliwa. 15. Vizuizi katika kujihusisha na madawa na vitu vya kulevya. 16. Adhabu kwa kumiliki, kununua kutengeneza n.k wa madawa ya kulevya n.k 17. Adhabu kuhusu umiliki, utumiaji wa madawa na vitu vya kulevya kwa kiwango kidogo. 18. Adhabu kwa kwenda kinyume na kifungu cha 17. 19. Adhabu kwa ubadhirifu kwa wakulima walioruhusiwa. 20. Adhabu kuhusiana na uvunjaji wa masharti, leseni au kibali. 21. Adhabu kuhusiana na kufadhili vitendo visiyo halali kisheria. 22. Adhabu kuhusiana na kusaidia utendaji kosa chini ya sheria hii. 23. Kujitayarisha kutenda kosa. 24. Adhabu kwa utendaji wa makosa baada ya hukumu ya awali. 25. Adhabu kwa kosa ambalo hakuna adhabu iliyowekwa. 26. Wajibu wa kuthibitisha 27. Makosa yasiyo na dhamana. 28. Makosa yanayotendwa na makampuni. 29. Kuachiliwa kwa watawaliwa kwa lengo la kuwapatia tiba. SEHEMU YA V UTARATIBU 30. Matumizi ya Sheria ya Mwenenendo wa Makosa ya Jinai na mabadiliko muhimu. 31. Utaratibu wa kushikilia pale ukamataji hauwezekani. 32. Jukumu la wamiliki wa ardhi kutoa habari ya mazao yaliyolimwa kinyume cha sheria. 33. Uwezo wa kushikilia mazao yaliyolimwa kinyume cha sheria. 34. Tume kuelekeza baadhi ya vitu kuangamizwa. 35. Uhusiano wa kauli katika mazingira fulani. 36. Dhana la umiliki wa vitu haramu. 37. Maofisa walioruhuisiwa kushikilia vifaa vilivyokamatwa. 38. Jukumu la maafisa mbalimbali kusaidiana. 39. Ukamataji na ushikiliwaji kuripotiwa katika muda wa saa arobaini na nane. 40. Adhabu kwa kuingia, kukamata, kushikiliwa kwa nia mbaya n.k.. 41. Adhabu dhidi ya maafisa wanaokataa kutenda wajibu wao au kusaidia watuhumiwa. 42. Uwezo wa kutaifisha vitu n.k kuhusiana na kosa. 43. Utaifishaji kama hakuna mashtaka. 44. Dhana ya kuwa ni nyaraka katika masuala fulani. 45. Uwezo wa afisa aliyeruhusiwa kutaka taarifa. 2

SEHEMU YA VI UKAMATAJI WA MALI ILYOTOKANA NA AU ILIYOTUMIWA KATIKA USAFIRISHAJI HARAMU 46. Ukamataji wa mali 47. Kukataza kushikilia mali iliyopatikana isivyo halali. 48. Kamishna kuruhusu uchunguzi au ukaguzi. 49. Wajibu wa kuthibitisha. 50. Malipo badala ya kutaifisha. 51. Rufani. 52. Uwezo wa kuchukua umiliki. 53. Mpangilio kuhusiana na kufautilia, kupata n.k wa mali. SEHEMU YA VII MASHARTI YA KAWAIDA 54. Ulinzi kwa kitendo kilichofanyika kwa nia njema. 55. Tume kuangalia mikataba ya kimataifa wakati wa kuandaa kanuni. 56. Mamlaka ya Serikali katika kuanzisha vituo n.k vya utambuzi wa tiba kwa watawaliwa na kutoa madawa ya kulevya. 57. Kiwango cha mamlaka. 58. Mamlaka ya Tume kutoa maelekezo. 59. Mamlaka ya kukasimu. 60. Mamlaka ya Serikali Kuu kuandaa kanuni. 61. Matumizi ya Sheria ya Ushuru wa Forodha (Uendeshaji na Viwango). 62. Matumizi ya Sheria ya Madawa na Sumu kuzuiwa. 63. Kuokoa nchi na sheria maalumu. 64. Kufuta na kuokoa. 65. (Imefutwa] 66. [Imefutwa] 67. [Marekebisho] MAJEDWALI 3

SURA YA 95 SHERIA YA MADAWA NA UZUIAJI WA USAFIRISHAJI WA MADAWA HARAMU Sheria ya kuunganisha sheria inazohusiana na madawa ya kulevya, kuweka masharti ya udhibiti na utendaji unaohusiana na madawa ya kulevya na vitu vya kulevya; kukamata mali iliyotokana na usafirishaji haramu wa madawa ya kulevya na vitu vya kulevya; kuzuia usafirishaji haramu wa madawa ya kulevya na vitu vya kulevya na kutekeleza masharti ya mkataba wa kimataifa wa madawa ya kulevya na vitu vya kulevya. Sheria Na: 9 ya 1995 9 ya 1996 17 ya 1996 31 ya 1997 9 ya 2002 SEHEMU YA I MASHARTI YA MWANZO [1Januari, 1996] [Gazeti la serikali Na. 10 la1996 na Jina fupi matumizi Tafsiri 31ya 1997 Jedw. 1.-(1) Sheria hii itaitwa Sheria ya Madawa na Uzuiaji wa Usafirishaji wa Madawa Haramu. (2) Katika Sheria hii,isipokuwa pale muktadha utakapohitaji vinginevyo- "mtawaliwa" maana yake ni mtu ambaye- (a) akipewa dawa anashindwa kujidhibiti kwa matumizi ya dawa hiyo;na (b) akiacha kutumia dawa kuna uwezekano wa mtu huyo kuona dalili za matatizo ya akili au uchovu wa mwili; "bangi maana yake ni sehemu yoyote ya mmea ukiacha mbegu,mmea uliokomaa, au nyuzinyuzi zinazotokana na mmea wa bangi; "mafuta ya bangi " maana yake majimaji yoyote yenye bangi kwa kiwango chochote; "mmea wa bangi " maana yake ni mmea wowote wa bangi kwa jina lolote na inajumisha sehemu yoyote ya mmea huo; 4

Sura ya 152 "utomvu wa bangi maana yake ni utomvu uliotengwa kupata utomvu usiosafishwa kutokana na mmea wa bangi; "kemikali tangulizi" maana yake ni kitu kinachotumika mara kwa mara katika utengenezaji haramu wa madawa ya kulevya au vitu vya kulevya kama ilivyotafsiriwa katika Ibara ya 12 ya Mkataba wa Kimataifa Unaopinga Matumizi ya Madawa na Vitu vya Kulevya vilivyotajwa katika orodha ya 1 na orodha ya 11 kama inavyoonyeshwa katika jedwali la pili la sheria hii; "jani la koka maana yake ni- (a) jani la mmea wa koka isipokuwa jani la kokeini ambalo (b) kokeini na alkaloidi imeondolewa; mchanganyiko wowote wenye na usio na kifaa lakini hautahusisha maandalizi yoyote yenye asilimia zaidi ya 0.1 ya kokeini; "mmea wa koka"maana yake ni mmea wa aina yoyote ya genus erythroxylon ; "Tume" maana yake ni Tume ya Wizara Mbalimbali ya Kuratibu Udhibiti wa Madawa iliyoanzishwa chini ya kifungu cha 4; "chombo cha uchukuzi" maana yake ni chombo cha uchukuzi cha maelezo yoyote na kinahusisha ndege,gari au meli; "mahakama kuhusiana na makosa chini ya vifungu vya 12 na 12(d) maana yake ni mahakama ya chini na kuhusiana na makosa chini ya vifungu vya 16,17,18,20,121,22 na 23 maana yake ni mahakama kuu; "kulima " inajumuisha kupanda,kusambaza mbegu,,kukopesha au kuvuna; "daktari wa meno" maana yake ni daktari wa meno aliyeruhusiwa na kupewa leseni ya kuchunguza,kutibu na kutoa tiba kwa magonjwa chini ya sheria ya madaktari na madaktari wa meno; "madawa" maana yake ni madawa ya kulevya na vitu vya kulevya vilivyoainishwa katika Jedwali; "usafirishaji haramu", kuhusiana na madawa ya kulevya maana yake ni - (a) (b) (c) (d) (e) kulima jani lolote la koka au kukusanya kiasi chochote cha koka; kulima afyumi au mmea wowote wa bangi; kujihusisha na uzalishaji,utengenezaji,umiliki uuzaji ununuzi,usafirishaji,utunzaji,usfungaji utumiaji uingizaji nchini,utoaji nje ya nchi wa madawa na vitu vya kulevya; kuhusika na utendaji wowote wa madawa au vitu vya kulevya; kupangisha jengo lolote kwa lengo la kutenda kazi zozote zaidi ya zile zilizoruhusiwa chini ya sheria au taratibu au amri yoyote au masharti ya leseni yoyote iliyotolewa na itajumuisha- (i) kugharamia moja kwa moja au vinginevyo kwa kazi yoyote ile iliyotajwa; (ii) kushiriki katika kuendeleza au kusaidia utendaji wa kazi yoyote iliyotajwa;na (iii) kuhodhi watu wanaojihusisha na kazi yoyote 5

Sura ya 152 Sura ya iliyotajwa; "mkataba wa kimataifa" maana yake ni- (a) ni mkatabaa wa pekee wa madawa ya kulevya,1961; (b) Itifaki inayorekebisha kifungu kidogo cha (a)iliyokubaliwa katika mkutano wa umoja wa mataifa huko Geneva Machi,1972; (c) mkataba wa vitu vya kulevya, 1971 uliokubaliwa na mkutano wa umoja wa maytaifa huko Vienna februari 1971; na (d) Mkataba wa Umoja wa Mataifa Dhidi ya Usafirishaji Harami wa Madawa ya Kulevya na Vitu vya Kulevya uliokubaliwa huko Vienna 19 Desemba,1988; na (e) mkataba mwingine wowote wa kimataifa au itifaki au hati nyingine inayorekebisha mkataba wowote wa kimataifa kuhusiana na madawa au vitu vya kulevya,ambao unaweza kukubaliwa na Jamhuri ya Muungano baada ya kuanza kutumika kwa sheria hii; kutengeneza kuhusiana na madawa au vitu vya kulevya inajumuisha- (a) hatua zote kuondoa uzalishaji amazo madawa au vitu hivyo vyaweza kupatikana; (b) kusahihisha madawa hayo au vitu ; (c) (d) kubadilisha madawa hayo au vitu;na utayarishaji wa (,usio wa duka la madawa)au kuwapo kwa dawa hizo au vitu; "dawa zilizotengenezwa maana yake ni- (a) vizalishi vyote vya koka,bangi ya tiba,vizalishi vya afyumi na mpopi ; (b) vitu vyovyote vya kulevya au utengenezaji ambao Tume inaweza,ikitilia maanani taarifa zinazopatikana kuhusiana na asili au uamuzi kama upo chini ya mkataba wa kimataifa, kwa notisi katika gazeti la serikali vimesemwa kutokuwa dawa za kutengeneza; "daktari wa tiba" maana yake ni tabibu au mpasuaji aliyekubaliwa na kuwa na leseni ya kuchunguza na kutoa tiba kwa wagonjwa chini ya sheria ya madaktari na madaktari wa meno; "bangi ya tiba maana yake ni zidua yoyote ya bangi; "madawa ya kulevya " maana yake ni kitu chochote kilichoainishwa katika jedwali au chenye viini vilivyoainishwa katika jedwali; "afyumi" maana yake ni- (a) juisi iliyoganda ya afyumi mpopi;na (b) mchanganyiko wowote ulio na au usio na kitu kisichoinjikwa, cha juisi ya mgando ya afyumi mpopi lakini haitajumisha matayarisho yoyote yenye zaidi ya asilimia 0.2 ya morfimi; "vizalishi vya koka maana yake ni- (a) bangi ya madawa, ambayo imepitia hatua muhimu kutumika kama dawa kufuatia mahitaji ya Sheria ya 6

219 Madawa na Sumu au madawa mengine yoyote yaliyoelekezwa na serikali katika unga au vinginevyo au kilichochanganywa na vitu visivyoinjikwa; (b) bangi iliyotengenezwa yaani zao lolote la bangi lililopatikana kwa utendaji ulioandaliwa kubadili bangi kuwa kitu kinachoweza kuvutwa na mabaki mengine baada ya bangi kuvutwa; (c) alkaloidi yaani morfimi,kodeini and chumvi zake; (d) alkaloidu inayojulikana kama heroini na chumvi zake;na (e) matayarisho yote yenye zaidi ya asilimia mbili ya mofimi ; "mofimi mpopi" maana yake ni- (a) (b) mmea wa aina ya papaver somniferum;na mmea wa aina ya papaver ambapo bangi au alkaloidi inaweza kupatikana na ambayo tume inaweza kwa notisi katika gazeti la serikali ikionyeshwa kuwa afyumi mpopi kwa madhumuni ya sheria hii; "mahali " inajumuisha ardhi tupu,majengo chombo cha baharini au ndege; "jani la mpopi" maana yake ni sehemu zote ukiondoa mbegu za afyumi mpopi baada ya kuvunwa ama katika hali ya uhalisia au ilyokatwa,sagwa au unga na kama ni au siyo juisi imetolewa huko; "kutayarisha", kuhusiana na madawa ya kulevya au vitu vya kulevya maana yake ni dawa au madawa au vitu hivyo katika hali ya uji au mchanganyiko ulio na moja au zaidi ya dawa au vitu hivyo; "uzalishaji" maana yake ni kutenganisha afyumi, jani la mpopi majani ya mpopi koka au bangi kutoka kwa mimea ambapo imetolewa; "mmea uliokatazwa" maana yake ni bangi, koka afyumi mpopi na papava setigerum; " vitu vya kulevya maana yake ni vitu vyovyote vya asili au kutengenezwa au kifaa chochote cha asili au chumvi au matayarisho ya vitu hivyo au vifaa vilivyojumuishwa katika orodha ya vitu vya kulevya katika jedwali; "uza" kunajumuisha kuonyesha au kuomba kununuliwa; "kutoa" kunajumuisha kusafirisha,kupeleka,kushusha kugawa na pia kuomba kugawa; "kusafirisha nje ya Jamhuri ya Muungano" maana yake kutoa ndani ya Jamhuri ya Muungano na kupeleka nje ya Jamhuri ya Muungano; "kuingiza ndani ya Jamhuri ya Muungano maana yake ni kuleta ndani ya Jamhuri ya Muungano kutoka nje ya Jamhuri ya Muungano na inajumuisha kuleta katika bandari yoyote au kiwanja cha ndege au mahali popote ndani ya Jamhuri ya Muuungao madawa ya kulevya au vitu vya kulevya hata kama havijatolewa kutoka chombo cha baharini, ndega, gari au chombo chochote cha usafirishaji ambacho kimeubeba; Kusafirisha maana yake ni kutoa toka sehemu moja kwenda kwingine ndani ya Jamhuri ya Muungano; "usafirishaji haramu" maana yake ni kuingiza nchini, kusafirisha nje ya 7

nchi,kutengeneza,kununua,mauzo,kutoa,kugawa,kutunza,kutumia,kus afirisha,kushusha au kugawa kwa mtu yeyote madawa ya kulevya au vitu vya kulevya au dawa au kitu kinachokuliwa kuwa ni dawa au kitu cha kulevya na mtu huyo lakini haitajumuisha- (a) uingizaji au usafirishaji nje wa dawa au kitu chochote cha kulevya au kumpelekea ombi la kununua kwa niaba ya mtu yeyote ambaye ana leseni chini ya sheria hii kulingana na masharti ya leseni; (b) kutengeneza, kununua, mauzo,kutoa, kugawa, kutumia. kusafirisha kutoa au kugawa dawa au kitu chochote cha kulevya au kumpelekea ombi la kununua kwa niaba ya mtu yeyote ambaye ana leseni chini ya sheria hii kufuatia masharti ya leseni; (c) (d) (e) kuuza au kugawa au kutumia kwa madhumuni ya tiba na kulingana na masharti ya sheria hii au kutoa ombi kwa tabibu au daktari wa wanyama mpasuaji au daktari wa meno au mtu mwingine yeyote mwenye sifa za kufanya hivyo chini ya ya maelekezo ya tabibu,daktari wa meno au wa wanyama mpasuaji; kuuza au kugawa kulingana na masharti ya sheria hii ya dawa au kitu chochote cha kulevya na mfamasia aliyesajiliwa; "kutumia" kuhusiana na madawa au vitu vya kulevya maana yake ni kitu chochote kilichoainishwa katika jedwali au kiini kingine chenye kuwa na kitu kilichoainishwa katika jedwali hilo; SEHEMU YA II KUUNDWA KWA TUME YA WIZARA MBALIMBALI YA KURATIBU UDHIBITI WA MADAWA Jukumu la Serikali la kuchukua hatua za kuzuia utumiaji mbaya wa dawa 3.-(1) Kufuatana na masharti ya sheria, Serikali itachukua hatua kama itakavyoona ni muhimu kwa lengo la kuzuia na kupambana na utumiaji mbaya wa madawa ya kulevya, vitu vya kulevya na usafirishaji haramu wake. (2) Hususani na bila kujali ujumla wa masharti ya kifungu kidogo cha (1),hatua ambazo Serikali inaweza kuchukua chini ya kifungu kidogo cha 1 itajumuisha hatua kuhusiana na yote au mojawapo ya masuala yafuatayo- (a) uratibu wa matendo ya baadhi ya maafisa na mamlaka chini ya sheria hii au chini ya sheria nyingine yoyote inayotumika kuhusiana na utekelezaji wa masharti ya sheria hii na majukumu chini ya mkataba wa kimataifa; (b) msaada kwa mamlaka husika katika nchi za nje na mashirika ya nje husika kwa nia ya kurahisisha uratibu na kitendo cha pamoja cha kuzuia na kugandamiza usafirishaji haramu wa 8

Kuundwa kwa tume ya taifa ya kuratibu udhibiti wa madawa madawa na vitu vya kulevya; (c) kutambua, kutibu, kuelimisha, kutunza, kukarabati na kuwajumuisha katika jamii waathirika; (d) mambo mengine kama ambavyo serikali itaona muhimu kwa lengo la kuwa na utekelezaji mzuri wa sheria hii na kuzuia na kupambana na utumiaji mbaya wa madawa na vitu vya kulevya na usafirishaji haramu. 4.- (1) Rais kwa amri katika gazeti la serikali ataunda Tume ya taifa ya udhibiti wa dawa ambayo itakuwa na jukumu la kutafsiri, kuendeleza na kuratibu sera ya Serikali ya udhibiti wa utumiaji mbaya wa dawa na usafirishaji haramu. (2) Rais kwa amri katika gazeti la serikali atamteua kamishna kwa lengo la kutekeleza sera ya Tume na uratibu wa kila siku wa Serikali kuhusiana na udhibiti wa utumiaji mbaya wa madawa. (3)Kamishna atasaidiwa na sekretariati ambayo itakuwa na wajumbe wasiozidi kumi na tano watakaochaguliwa na Tume. (4) Sekretariati itamshauri kamishna kuhusiana na mambo ya utekelezaji wa sheria kama yatakavyopelekewa kwa kamishna na Tume (5) Kamishna ataandikisha maafisa wengine kwa vyeo kama atakavyoona inafaa. (6) Tume chini ya uenyekiti wa Waziri Mkuu itakuwa na wafuatao_ (a) Waziri anayehusika na masuala ya sheria; (b) Waziri anayehusika na masuala ya mambo ya ndani; (c) Waziri anayehusika na afya; (d) Waziri anyehusika na maendeleo ya jamii; (e) Waziri anayehusika na mambo ya nchi za nje; (f) Waziri anayehusika na fedha; (g) Waziri anayehusika na maendeleeo ya vijana; (h) Waziri wa nchi (ofisi ya waziri kiongozi-zanzibar; (i) Waziri anayehusika na utalii Zanzibar; (j) (k) Waziri wa nchi mipango(zanzibar); na Wajumbe wengine watendaji katika udhibiti wa matumizi mabaya ya dawa; (7) Mawaziri wengine wanaweza kuitwa kutumika katika Tume kutegemea na ajenda na Tume inaweza kumualika mtu mwingine yeyote kuhudhuria kama itaona muhimu kumualika mtu (8) Tume itakutana angalau mara mbili kwa mwaka katika kikao cha kawaida na wakati wowote muhimu kwa kikao maalumu. (9) Pale ambapo Waziri Mkuu atashindwa kufanya kazi zake chini ya sheria hii kwa sababu yoyote ile Waziri anayehusika na mambo ya sheria ndiye atakuwa mwenyekiti, na asipokuwepo Waziri anayehusika na masuala ya mambo ya ndani, naye asipokuwepo Waziri anayehusika na afya. Kazi za Tume 5.-(1) Kazi za Tume zitakuwa ni kutafsiri, kuendeleza na kuratibu sera ya serikali ya udhibiti wa utumiaji mbaya wa madawa na usafirishaji, 9

haswa katika- (a) kuendeleza na kutekeleza mpango wa kitaifa wa udhibiti wa dawa; (b) kutekeleza masharti ya mikataba ya kimataifa ya dawana vitu vya kulevya; (c) (d) (e) (f) (g) (h) (i) (j) kuhuisha na kutohoa sheria na kanuni za udhibiti wa dawa; kuendeleza uzuiaji wa utumiaji mbaya wa dawa na taarifa kwa umma kwa vijana, familia, maprofesa, waalimu na umma kwa ujumla kwa kusaidia mipango katika fani ya habari na uzuiaji; kuundwa kwa mfumo wa ukusanyaji wa data na mfumo wa uchambuzi katika hatua ya kitaifa kuhusu matumizi mabaya ya dawa na usafirishaji wa dawa; kuendeleza tiba na programu za ukarabati kwa waathirika; kufanya utafiti wa utawaliwa wa dawa; mafunzo ya watu wanaosimamia hatua zinazohusika na utumiaji mbaya wa dawa na usafirishaji mbaya wa dawa na wahusika na fedha haramu; kuendeleza na kuhakikisha ushirikiano wa kimataifa; kuhakikisha uratibu na msaada wa shughuli za taasisi zisizo za kiserikali na vyama vinavyojishughulisha na matumizi mabaya ya dawa; (2) Tume itahakikisha kwamba mahitaji ya mikataba ya kimataifa yanatimizwa vizuri na Serikali katika ngazi ya taifa na katika uhusiano wake na nchi zingine, na vyombo vya kimataifa vinavyosimamaia udhibiti wa dawa pamoja na utekelezaji katika ngazi ya taifa na ya kimataifa ya vyombo vya udhibiti wa dawa Ripoti ya Tume kuwasilishw a bungeni Bajeti ya Tume 6. Tume itachapisha kila mwaka ripoti inayoelezea hali halisi ya taifa na maendeleo yake kuhusiana na upatikanaji na uhitaji wa dawa na kuandaa mapendekezo yanayoweza kuendeleza kupiga vita matumizi mabaya ya madawa na ripoti hiyo kuwasilishwa Bungeni. 7.-(1) Tume itakuwa na bajeti yake yenyewe ya kumsaidia Kamishna na shughuli zingine maalum, hafla maalum zitakazofanywa na ofisi za umma na taasisi, pamoja na mashirika, vyama na wahusika binafsi katika jitihada za udhibiti wa matumizi mabaya ya dawa. (2) Fedha za bajeti ya Tume zitatokana na - (a) kiasi cha fedha kinachotolewa kwa Mfuko na Bunge ; (b) mali na thamani iliyokamatwa kutoka kwa wasafirishaji wa dawa na kupewa mfuko wa taifa wa udhibiti wa utumiaji mbaya wa dawa ulioanzishwa chini ya kifungu cha 11; (c) misaada inayotolewa kawa mfuko na ushirikiano wa serikali mbalimbali na taasisi zisizo za serikali zinazojishughulisha na jitihada za udhibiti wa dawa. (3) Tume itasimamia ugawaji na utumiaji wa fedha na kamishna na itasimamia mfuko wa taifa wa matumizi mabaya ya dawa. 10

(4) Pale mali zimetolewa kwa mfuko, Tume itaamua juu ya ugawaji kwa umma au chombo binafsi kinachosimamia udhibiti wa matumizi mabaya ya dawa kutegemea asili ya mali na uhitaji wa taasisi husika. Kamishan kuhusika katika mikutano ya wahusika wa wizara mbalimbali. Kamishna ataandaa maamuzi na kuhakikisha utekelezaji Tume kutumia fedha kwa mahitaji mablimbali 8. Kamishna atahusika katika mikutano ya wahusika wa Wizara mbalimbali. 9. Kamishna ataandaa maamuzi ya Tume na kuhakikisha yanatekelezwa bila kujali yaliyotangulia,kamishna - (a) ataiwakilisha Tume katika mamlaka za kimataifa zilizo mahiri katika masuala ya udhibiti wa dawa ; (b) atatia moyo na kuratibu shughulli za wizara husika ; (c) atahakikisha mawasiliano yanayofaa na mashirika ya kimataifa na kuhakikisha au kusaidia usambazaji wa taarifa na data kwa vyombo mahiri vya kimataifa kama inavyotakiwa na mikataba; 10. Tume itatumia fedha kwa mipango mbalimbali ili kutimiza mahitaji maalum ya idara za serikali, taasisi za umma, au ofisi za umma,vyama au wahusika binafsi katika kutekeleza maamuzi yake. SEHEMU YA III MFUKO WA UDHIBITI WA MATUMIZI MABAYA YA MADAWA Kuanzish wa kwa mfuko 11.-(1) Tume itatoa notisi itakayo chapishwa katika gazeti la serikali, ya kuunda mfuko utakaojulikana kama mfuko wa udhibiti wa matumizi mabaya ya dawa na utaidhinishiwa- (a) (b) (c) (d) kiasi cha fedha kilichotolewa na Bunge; mauzo ya vitu vinavyotokana na mali iliyokamatwa chini ya sehemu ya VI; misaada ambayo inaweza kutolewa na mtu yeyote au taasisi yoyote; kipato chochote kinachotokana na uwekezaji wa kiasi kilichoidhinishiwa kwenye mfuko chini ya masharti ya sheria hii. (2) Mfuko utatumiwa na Tume kugharamia matumizi yaliyofanyika yanayohusiana na hatua zilizochukuliwa kupambana na usafirishaji haramu katika au udhibiti wa utumiaji mbaya wa madawa na vitu vya kulevya. (3) Kamishna ataishauri Tume kuhusu na matumizi ya mfuko 11

SEHEMU YA IV KATAZO LA UMILIKI NA USAFIRISHAJI WA MADAWA NAVITU VYA KULEVYA NA ULIMAJI WA MIMEA FULANI Ukatazo wa ulimaji wa mimea fulani na vitu Sheria Na 31 ya 1997 Jedw. 12. Mtu yeyote- (a) atakayelima bangi,mmea wakoka au kukusanya sehemu yoyote ya mmea wa koka; (b) atakayelima afyumi mpopi au papaver setigerum; (c) anayemiliki, anayeishi au anayeshughulikia uendeshaji wa jengo lolote, akiruhusu majengo kutumika kwa ulimaji, ukusanyaji au uzalishaji wa dawa yoyote iliyotajwa katika aya ya (a) na (b) ; (d) atazalisha, atamiliki, atasafirisha, ataingiza katika Jamhuri ya Muungano, atauza, atanunua atatumia au kufanya jambo lolote linalohusiana na jani la mpopi, mmea wa koka, jani la koka, afyumi iliyotengenezwa, afyumi mpopi, bangi, dawa iliyotengenezwa au mchanganyiko wenye dawa iliyotengenezwa, kitu cha kulevya,dawa ya kulevya, kitendo hicho au kutotenda huko ni sawa na uvunjaji wa masharti ya sheria hii au taratibu au amri chini ya sheria hii, atatenda kosa na akihukumiwa atatakiwa kulipa faini ya shilingi milioni moja au mara tatu ya bei ya soko ya mmea uliokatazwa, kutegemea kilicho kikubwa zaidi, au kifungo cha muda usiozidi miaka ishirini au kwa vyote faini na kifungo. Uwezo wa Tume kuruhusu na kusimamia ulimaji, uzalishaji au uuzaji n.k wa afyumi, majani ya koka n.k. 13.-(1) Kufuatana na masharti ya kifungu cha 12,Tume inaweza kwa kanuni- (a) kuruhusu na kusimamia- (i) ulimaji,au ukusanyaji (kiasi chochote tu kwa ajili ya Serikali) ya m mea wa koka,uzalishaji umiliki,uuzaji,ununuzi, usafirishaji uingizaji ndani ya Jamhuri ya Muungano,utumiaji wa majani ya koka;au (ii) ulimaji, na (ulimaji huo kwa ajili tu 12

ya serikali ) wa afyumi mpopi; au (iii) uzalishaji na utengenezaji wa afyumi na uzalishaji wa jani la afyum;au (iv) uuzaji wa afyumi na vizalishi vya afyumi kutoka katika viwanda vya Serikali kwa uuzaji nje ya Jamhuri ya Muungano au kwa wakemia wazalishaji;au (v) utengenezaji wa madawa ya kutengeneza (zaidi ya mpopi uliotengenezwa) lakini hautajumuisha utengenezaji wa mpopi wa dawa au maandalizi yoyote yaliyo na dawa za kutengeneza kutoka kwenye vifaa ambavyo mtengenezaji anaruhusiwa kihalali kumiliki; au (vi) utengenezaji,umiliki,usafirishaji,uu zaji,ununuzi,utumiaji wa vitu vya kulevya;au (vii) uingizaji ndani ya Jamhuri ya Muungano na usafirishaji majini wa madawa na vitu vya kulevya; (b) kuagiza jambo lingine lolote linalofaa ili kufanya udhibiti wa serikali juu ya masuala yaliyoainishwa chini ya aya ya (a) juu. (2) Bila ya kuathiri Mamlaka yaliyotolewa chini ya kifungu kidogo cha (1), amri inaweza kutolewa na Tume kuhusu uendeshaji wa leseni, vibali au vinginevyo uzalishaji, utengenezaji, umiliki, usafirishaji, uingizaji, upelekajikutoka Jamhuri ya Muungano, uuzaji, utumiaji, utunzaji, usambazaji, uharibifu au upatikanaji wa dawa yoyote au kitu cha kulevya. Madawa ya kulevya na vitu vya kulevya kutokamatwa Vizuizi juu ya madawa na vitu vya kulevya 14. Bila ya kujali jambo lolote kinyume na sheria yoyote au mkataba, hakuna dawa ya kulevya, dawa, kitu cha kulevya au mmea uliokatazwa, haitatakiwa kushikiliwa na mtu yeyote kwaajili ya upatikanaji wa fedha yoyote chini ya amri yoyote ya mahakama au mamlaka yoyote au vinginevyo. 15. Mtu yeyote wa Jamhuri ya Muungano asijihusishe na au kuendasha biashara yoyote ya madawa au vitu vya kulevya vinapatikana nje ya Jamhuri ya Muungano au kutolewa kwa mtu yeyote nje ya Jamhuri ya 13

Muungano isipokuwa kwa kibali au ruhusa ya Tume na kwa masharti yanayoweza kuwekwa na Tume. Adhabu kwa umiliki, ununuzi, utengenezaji n.k wa dawa za kulevya n.k. 16.-(1) Mtu yeyote ambaye- (a) atamiliki au atafanya kitendo chochote kuhusiana na dawa za kulevya au mchanganyiko wenye madawa za yaliyotengenezwa atatenda kosa na akihukumiwa atatakiwa kulipa faini ya shilingi milioni kumi au mara tatu ya bei ya soko ya dawa za kulevya au mchanganyiko wowote uliyo na dawa za zilizotengenezwa au kilicho kikubwa zaidi au kifungo cha maisha au kwa vyote faini na kifungo; (b) atasafirisha dawa au kitu chochote cha kulevya au kitu kilichotolewa au kilichosemwa kuwa ni dawa au kitu cha kulevya atatenda kosa na akihukumiwa atatakiwa- (i) kuhusiana na dawa yoyote au kitu chochote cha kulevya faini ya shilingi milioni kumi au mara tatu ya bei ya soko la dawa au kitu cha kulevya, ambacho ni kikubwa, na kuongezea hilo, kifungo cha maisha lakini si kwa wakati wote iwe pungufu ya miaka ishirini; (ii) kuhusiana na vitu vyovyote vingine zaidi ya dawa ya kulevya au kitu cha kulevya ambacho kilichotolewa au kusemwa kuwa ni madawa au vitu vya kulevya kwa faini isiyopungua shilingi milioni moja na nyongeza ya kifungo cha maisha lakini si wakati wote itakuwa pungufu ya miaka ishirini. (2) mtu yeyote ambaye- (a) anavuta, ananusa au vinginevyo anatumia madawa au vitu vyovyote vya kulevya; (b) bila uhalali na sababu ya kuridhisha atakutwa katika nyumba yoyote chumba au mahali kwa lengo la kuvuta, kunusa au vinginevyo anatumia madawa au vitu vya kulevya ; (c) atakuwa anamiliki au yumo au anaendesha jengo lolote au anasafirisha, anaruhusu litumiwe kwa lengo la- (i) kutayarisha afyumi kwa kuvuta au 14

(d) kuuza au kuvuta, kunusa au vinginevyo kutumia madawa au vitu vyovyote vya kulevya; au (ii) kutengeneza,kuzalisha,kuuza au kuvuta,kunusa au vinginevyo kutumiwa kwa madawa au vitu vyovyote vya kulevya; au ana katika umiliki bomba lolote au chombo kingine kwa matumizi yanayohusiana na uvutaji, unusaji au vinginevyo kutumia afyumi, bangi, heroini au koka au chombo chochote kilichotumika kuhusiana na uvutaji, unusaji au vinginevyo kutumia afyumi, bangi, heroni au koka au chombo chochote kinachotumika katika kutengeneza afyumi au dawa nyingine yoyote au kitu cha kulevya kwa kuvuta, atatenda kosa na akihukumiwa atatakiwa kulipa faini ya shilingi milioni moja au kifungo cha miaka kumi au vyote faini na kifungo Adhabu kuhusiana na umiliki, utumiaji wa kiasi kidogo cha madawa au vitu vya kulevya 17.-(1) Mtu yeyote ambaye amekwenda kinyume na masharti ya sheria hii au taratibu yoyote au amri iliyotayarishwa chini ya sheria hii, anakuwa na kiasi kidogo cha dawa au kitu chochote cha kulevya ambacho kimethibitika kilikuwa kinatakiwa kutumiwa na mtu binafsi na si kwa kuuza au kugawa,au kutumia dawa au kitu chochote cha kulevya, atatakiwa bila ya kujali mambo mengine katika sehemu hii atawajibika - (a) ikiwa dawa au kitu cha kulevya iliyomilikiwa au kutumiwa ni kokeini, mofimi au dawa au kitu kingine chochote cha kulevya, kilichoainishwa na Tume katika notisi iliyochapishwa katika gazeti la Serikali, kutoa faini ya shilingi laki tatu au kifungo cha miaka kumi au vyote faini na kifungo; (b) iwapo dawa au kitu cha kulevya kinachomilikiwa au kutumiwa ni kile ambacho hakijaainishwa chini ya aya ya (a),kutoa faini ya shilingi laki mbili au kifungo cha kipindi cha miaka saba au vyote faini na kifungo (2) kulingana na kifungu kidogo cha (1), kiasi kidogo kwa madhumuni ya kifungu hiki maana yake ni kiasi chochote ambacho kwa kanuni zilizochapishwa 15

katika gazeti la serikali kimeainishwa na Tume. (3) Endapo mtu atakutwa anamiliki dawa za kulevya au vitu vya kulevya, jukumu la kuthibitisha kwamba ilikuwa ni kwaajili ya matumizi binafsi ya mtu huyo, na siyo kwa kuuza au kugawa itakuwa kwa mtu huyo. Adhabu ya kwenda kinyume na kifungu cha 17 Adhabu kwa ubadhirifu wa wakulima walioruhusiwa Adhabu kuhusiana na kuvunja masharti ya leseni au kibali 18. Mtu yeyote ambaye- (a) (b) (c) anatumia dawa au kitu cha kulevya au anasababisha au anaruhusu itumike isipokuwa pale mtu aliyeruhusiwa na tabibu au daktari wa meno anayefanya kazi yake na kufuatana na maadili yaliyopo na kiwango au utaratibu wa kitaalamu; anaruhusu; au anaongezea dawa au kitu cha kulevya kwenye chakula au kinywaji bila ya mtumiaji kufahamu; au kuuza, kugawa au kupata dawa au kitu cha kulevya kwa kuonyesha maelezo huku akijua au akiwa na sababu za kuamini kwamba maelezo hayo yamegushiwa, yamepatikana isivyo halali au yametolewa zaidi ya miezi sita kabla ya kuwasilishwa, anatenda kosa na akihukumiwa atatakiwa kulipa faini ya shilingi milioni tano, au kifungo cha miaka thelathini au vyote faini na kifungo. 19. Mtu yeyote aliyepewa leseni ya kulima afyumi mpopi kwa ajili ya serikali,ambaye atafanya uharibifu au vinginevyo ataharibu visivyo halali afyumi iliyozalishwa au sehemu yoyote, atatenda kosa na akishtakiwa atatakiwa kulipa faini ya shilingi milioni tano au kifungo cha miaka isiyozidi thelathini au vyote, faini na kifungo na mahakama inaweza kwa sababu zinazotakiwa kurekodiwa katika hukumu kutoa faini inayozidi shilingi milioni tano 20. Pale mwenye leseni, kibali au ruhusa aliyopewa kufuatana na masharti ya sheria hii na kanuni au amri zilizotolewa chini ya sheria hii- (a) anaacha bila sababu ya msingi kuweka mahesabu au kutoa marejeo kulingana na sheria hii au taratibu zake ;au (b) anashindwa kutoa bila sababu ya msingi kuweka mahesabu au kutoa marejesho 16

kulingana na sheria hii au taratibu ziliozowekwa;au (c) anaweka mahesabu au taarifa ambayo ni ya uongo au ambayo anafahamu au ana sababu ya kuamini kuwa si sahihi;au (d) kwa kukusudia na kwa kujua anatenda kitendo chochote cha kuvunja sharti lolote la leseni, kibali au ruhusa ambalo adhabu imewekwa katika sehemu nyingine ya sheria hii, anatenda kosa na akihukumiwa atatakiwa kulipa faini ya shilingi milioni tano au kifungo cha kipindi cha miaka thelathini au kwa vyote, faini na kifungo. Adhabu kuhusiana na kufadhili vitendo visivyo halali Adhabu kuhusiana na kusaidia utendaji wa makosa chini ya sheria hii 21. Mtu yeyote kwa kujua moja kwa moja au kwa kuzunguka analipia fedha kitendo chochote kilichoainishwa katika aya za (a) mpaka (f) ya kifungu cha 16, au anamhifadhi mtu yeyote anaye jishughulisha na vitendo vilivyotajwa, anatenda kosa na akihukumiwa atatakiwa kulipa faini ya shilingi milioni tano au kifungo cha maisha. 22. Bila ya kujali kitu kingine chochote katika sheria nyingine yoyote, mtu yeyote ambaye- (a) atashirikiana na mtu mwingine yeyote; au (b) atashawishi, atashauri, atasaidia au ataficha au kujaribu kuficha kushawishi kushauri, mtu mwingine yeyote kutenda; au (c) atasababisha au atajaribu kusababisha (d) utendaji wa kosa chini ya sheria hii; au moja kwa moja au kwa kuzunguka anahusika na utendaji wa kosa chini ya sheria hii, anaweza kushitakiwa, kusikilizwa, kuhukumiwa na kuadhibiwa katika namna zote kama vile alikuwa mkosaji mkuu. Kujiandaa au kujaribu kutenda kosa 23. Ikiwa mtu atajiandaa kutenda au kutotenda kitu chochote ambacho ni kosa chini ya sehemu hii na kutokana na mazingira ya jambo inaweza kueleweka kwamba alikuwa amedhamiria kutenda kosa hilo lakini akazuiliwa na mazingira bila kupenda kwake, atapewa adhabu ya kifungo kisichopungua nusu ya kiwango cha juu cha muda, ambacho angekuwa ameadhibiwa kama 17

angetenda kosa hilo, na pia faini isiyopungua nusu ya kiwango cha juu ambayo angelipa kama angeadhibiwa, kama angetenda kosa hilo. Adhabu kwa kutenda kosa baada ya hukumu iliyopita Adhabu kwa makosa ambayo adhabu haijatolewa Wajibu wa kuthibitisha sheria Na:31 ya 1997 ; 9 ya 2002 Jedw Makosa yasiyokuwa na dhamana sheria na:9 ya 1996 Jedw Sheria na 9 ya 2002 Jedw. 24.-(1) Mtu yeyote atakayehukumiwa kwa makosa chini ya vifungu vya 16, 17, 20, 21 na 22 kwa kosa la pili na kila kosa litakalofuata atatakiwa kulipa faini ya shilingi milioni kumi au kifungo cha maisha. (2) Pale mtu atahukumiwa na mahakama halali nje ya Jamhuri ya Muungano chini ya sheria yoyote inayoendana na vifungu vya 16, 17, 20, 21 na 22, kulingana na hukumu hiyo, mtu huyo atashughulikiwa na kifungu kidogo (1) cha kifungu hiki kama vile amehukumiwa na mahakama ndani ya Jamhuri ya Muungano. 25. Mtu yeyote ambaye atakwenda kinyume na kifungu chochote cha sheria hii au amri au taratibu zilizoandaliwa au sharti lolote la leseni, kibali au ruhusa iliyotolewa chini ya sheria hii, ambapo hakuna adhabu tofauti iliyotolewa chini ya Sehemu hii, akihukumiwa atatakiwa kulipa faini isiyozidi shilingi milioni tano au kifungo kisichopungua muda wa miaka thelathini au vyote faini na kifungo. 26.- (1) Katika shtaka lolote kwa kosa la kuwa na kumiliki, kujishughulisha na kusafirisha, kuuza, kulima, kununua, kutumia, kulipia dawa au kitu chochote cha kulevya na wajibu wa kuthibitisha kwamba dawa au kitu cha kulevya hicho kilimilikiwa, kilishughulikiwa, kilisafirishwa, kiliuzwa, kililimwa, kilitumiwa au kililipiwa kufuatana na sharti la leseni, kibali au ruhusa iliyotolewa chini ya sheria hii, kanuni, taratibu au amri zilizoandaliwa chini ya sheria hii, utakuwa kwa mtu anayeshtakiwa. (2) Bila ya kuathiri masharti ya kifungu kidogo cha (1).itakuwa ni utetezi kwa mtu yeyote aliyeshitakiwa kwa kosa linalohusu umiliki wa dawa au kitu cha kulevya iwapo ataithibitisha mahakama na kuiridhisha kwa kuangalia mazingira ya kesi kwamba umiliki wa dawa au kitu hicho ulikuwepo bila ufahamu. 27.-(1) Afisa polisi anayesimamia kituo cha polisi, au mahakama ambayo mtuhumiwa ameletwa hatampa dhamana mtu huyo iwapo- 18

Sura ya 20 Makosa ya makampuni Kuachiwa kwa baadhi ya watawaliwa kwa lengo la kupatiwa tiba (a) mtu huyo ametuhumiwa kwa kosa linahusu usafirishaji haramu wa madawa au vitu vya kulevya lakini kwa kuzingatia mazingira yote ya kutendwa kwa kosa haikuwa kwa madumuni ya kusafirisha au kibiashara; (b) mtu huyo ameshtakiwa kwa kosa linalohusika na heroini, afyumi mpopi kokeni, jani la mpopi, mmea wa koka, majani ya koka, bangi au dawa au kitu kingine chochote kilichoainishwa katika jedwali katika sheria hii chenye thamani iliyothibitishwa na Tume ya taifa ya kuratibu uthibiti wa madawa isiyozidi shilingi milioni kumi. (2) Masharti ya kutoa dhamana yaliyoainishwa katika kifungu cha 148 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai itatumika sawasawa kwa makosa yote yenye kupata dhamana chini ya sheria hii. 28.-(1) Endapo kosa chini ya sheria hii limetendwa na kampuni, kila mtu ambaye wakati wa utendaji wa kosa alikuwa anasimamia kampuni katika biashara atachukuliwa kuwa ametenda kosa na atatakiwa kushitakiwa na kuadhibiwa ipasavyo. (2) Maelezo yoyote yaliyo katika kifungu kidogo cha (1) hayatampata mtu yeyote aadhibiwe ikiwa atathibitisha kwamba kosa lilitendwa bila yeye kujua au alijitahidi kuwa makini kuzuia kosa lisitendeke (3) Bila kuathiri kifungu kidogo cha (1), pale kosa lolote chini ya sehemu hii limefanywa na kampuni na ikathibitika kwamba kosa limefanywa kwa kibali au limesababishwa na uzembe wa mkurugenzi, katibu au afisa mwingine wa kampuni itachukuliwa kuwa kampuni inahitaji kushtakiwa na kuadhibiwa ipasavyo. 29.-(1) Pale muathiriwa yeyote atayetiwa hatiani kwa kosa chini ya kifungu cha 19 na mahakama husika inaona kwa kuzingatia umri, tabia, wasifa au hali ya kimwili na kiakili ya mtuhumiwa kwamba ni muhimu kufanya hivyo bila kuathiri sheria hii au sheria nyingine yoyote, mahakama inaweza badala ya kumhukumu kifungo chochote, kwa ridhaa yake aachiliwe ili apate tiba kutoka hospitali au taasisi inayotambuliwa na Serikali kwa kuweka dhamana katika fomu iliyoelekezwa na Tume akiwa na wadhamini au bila ya wadhamini ataelekezwa kwenda mahakamani na kutoa ripoti katika kipindi 19

kisichozidi miezi mitatu, ripoti inayohusu matokeo ya tiba yake na wakati huohuo kuacha kutenda kosa lolote chini ya Sehemu hii. (2) Pale mtuhumiwa anaposhindwa kutii masharti ya kuacha kutenda kosa baada ya mtuhumiwa kuachiwa na mahakama kwenda kupata tiba kufuatana na kifungu kidogo cha (1), mahakama inaweza kuamuru mtuhumiwa afike mahakamani ili aweze kuhukumiwa. Matumizi ya Sheria ya Mwenendo wa Kesi za Jinai na mabadiliko muhimu Utaratibu wa ukamataji pale utaifishaji hauwezekani SEHEMU YA V UTARATIBU 30.-(1) Masharti ya sheria yoyote ya Jamhuri ya Muungano kuhusiana na ukamataji, ukaguzi na madaraka ya kawaida na wajibu wa uchunguzi wa maafisa polisi, forodha, na mapato au mtu mwingine yeyote mweneye uwezo wa kukamata yatatumika katika sheria hii. (2) Kufuatana na kifungu kidogo cha (1), afisa yeyote aliyotajwa katika kifungu kidogo cha (1) anaweza wakati wowote- (a) kuingia na kukagua jengo lolote,usafiri au mahali; (b) kama anazuiwa, kuvunja mlango wowote au kuondoa kizuizi chochote katika kuingia huko; (c) kukamata madawa au kitu chochote kinachotengenezwa na vifaa vilivyotumika katika kutengeneza na kitu chochote au usafiri ambao yeye ana sababu za kuamini vimetumika katika kutenda kosa lolote chini ya sheria hii. (3) Pale afisa anapochukua taarifa kwa maandishi chini ya kifungu kidogo cha (2) au anaweka kumbukumbu, kuamini atatuma nakala yake kwa mkubwa wake wa kazi (4) Masharti ya kifungu hiki yatatumika kwenye makosa chini ya sehemu ya IV na kuhusiana na mmea wa mkoka, afyumi, mpopi au mmea wa bangi na pia kwa madhumuni haya, marjeo yatafanyika katika vifungu hivyo kwa madawa au vitu vya kulevya itatafsiriwa kujumuisha mmea wa mkoko, afyumi mpopi na mmea wa bangi. 31. Pale inapokuwa si rahisi kukamata mali yoyote ikiwemo mazao ambayo yanatakiwa kutaifishwa chini ya sheria hii, afisa yeyote aliyeruhusiwa chini ya kifungu cha 30 anaweza kumpa amri mwenye mali au mmiliki wa mali, kwamba asiondoe, asioondoke au asitumie mali bila ya kibali cha afisa huyo. 20

Wajibu wa wenye ardhi kutoa taarifa juu ya mimea iliyolimwa kinyume cha sheria Uwezo wa kushikilia mazao yaliyolimwa kinyume cha sheria Tume kuelekeza vitu fulani kuharibiwa 32.Kila mwenye ardhi atatakiwa kutoa taarifa mapema kwa afisa yeyote wa polisi au afisa yeyote wa idara zilizotajwa chini ya kifungu cha 30 juu ya afyumi mpopi, mmea wa bangi au mmea wa mkoka ambao unaweza kuwa umelimwa kinyume cha sheria kwenye ardhi yake na kila mwenye ardhi ambaye ameacha kutoa taarifa hiyo huku akijuwa, atachukuliwa kuwa ametenda kosa, na akihukumiwa atatakiwa kulipa faini ya shilingi milioni tano au kifungo cha miaka thelathini. 33. Afisa yeyote chini ya sheria hii anaweza kuamuru kushikiliwa kwa afyumi, mpopi, mmea wa bangi au mmea wa mkoka ambao yeye anaamini kuwa umelimwa kinyume cha sheria na anaweza kuamuru hivyo akijumuisha amri ya kuharibu zao kama atakavyoona inafaa. 34.-(1) Tume inaweza, ikizingatia hatari ya dawa au kitu chochote cha kulevya, uwezekano wa kuibiwa, kubadilishwa, ugumu wa mahali pa zuri pa kutunzia, nafasi au sababu zingine muhimu kwa notisi iliyotangazwa chini ya gazeti la serikali kuainisha dawa au kitu cha kulevya mara zinapokamatwa kuharibiwa na afisa huyo kwa namna ambayo Tume itaamua mara kwa mara, baada ya kufuata utaratibu uliainishwa. (2) Pale dawa au kitu chochote cha kulevya kinapokamatwa na afisa, afisa huyo atatayarisha ya madawa au vitu vya kulevya kuelezea kiasi chake,namna ya ufungaji, alama, namba au taarifa nyingine za utambuzi wa madawa au vitu hivyo vya kulevya na ufungaji wake, nchi vilipotokea na taarifa zingine, ama afisa huyo atakavyoona inafaa chini ya sheria hii na atatuma maombi kwa hakimu yeyote mwenye mamlaka chini ya sheria hii, kwa madhumuni ya - (a) kuthibitisha uhalisia wa orodha iliyotayarishwa;au (b) kuchukua mbele ya hakimu,picha za madawa au vitu na kuthibitisha kama picha hizo ni halisi; au (c) kuruhusu kuchukua sampuli za madawa au vitu mbele ya hakimu na kuthibitishwa uhalisia wa sampuli zilizochukuliwa. (3) Pale ombi limefanyika chini ya kifungu kidogo cha (2) hakimu atalikubali mapema iwezekanavyo ombi hilo. (4) Bila ya kuathiri chochote kilichopo chini ya 21

Sura ya 6 Sura ya 20 Uhusika wa taarifa chini ya mazingira fulani Dhana ya umiliki wa vitu haramu Maafisa walioruhusiwa kusimamia vifaa Sheria ya Ushahidi au Sheria ya Mwenendo wa Jinai, kila mahakama inayosikiliza kosa chini ya sheria hii itachukulia picha za madawa na vitu vya kulevya na sampuli zilizochukuliwa chini ya kifungu kidogo cha (2) na kuthibitishwa na hakimu, kama ushahidi mkuu kuhusiana na kosa hilo. 35. Taarifa iliyoandaliwa na kusainiwa na mtu mbele ya afisa yeyote aliyeruhusiwa chini ya kifungu cha 29 kwaajili ya upelelezi wa makosa, wakati wa uchunguzi au mwenendo wa afisa huyo, itahusika kwa lengo la kuthibitisha shtaka la kosa chini ya sheria hii,ukweli wa jambo utakuwa na- (a) pale mtu aliyetoa taarifa anapofariki au hapatikani au hawezi utoa ushahidi au amezuiliwa na mhusika wa upande mwingine au uwepo wake unakuwa mgumu bila ya kuchelewa au gharama, chini ya kulingana na mazingira ya kesi, mahakama itaona si muhimu ;au (b) pale mtu aliyeandaa taarifa anapohojiwa kama shahidi katika kesi iliyo mbele ya mahakama na mahakama inaona kuwa kulingana na mazingira ya kesi taarifa itabidi ipokelewe kama ushahidi kwa madhumuni ya utendaji wa haki 36. Kesi chini ya sheria hii, zitachukuliwa kwamba mtuhumiwa amendenda kosa mpaka kinyume chake kithibitike chini ya sehemu ya IV kuhusiana- (a) (b) na dawa au kitu chochote cha kulevya; afyumi mpopi yoyote, mmea wa bangi au mmea wa mkoka unaoota katika ardhi yoyote aliyolima; (c) chombo chochote kilichotengenezwa maalum au kundi la vyombo maalum vilivyochukuliwa kwa utengenezaji wa dawa au kitu chochote chea kulevya; au (d) vifaa vyovyote vilivyopitia mchakato wowote kwa ajili ya utengenezaji wa dawa au kitu cha kulevya, au mabaki yoyote kutokana na dawa au kitu chochote cha kulevya yaliyotengenezwa, kwa umiliki ambapo anashindwa kuuelezea vizuri. 37.-(1) Afisa aliyeruhusiwa chini ya kifungu kidogo cha (2) cha kifungu cha 30 atasimamia na kutunza, 22

vilivyokamatwa Wajibu wa maafisa mbalimbali wa kusaidiana Ukamataji na ushikiliaji utolewe taarifa katika muda wa saa arobaini na nane vifaa vyote vilivyokamatwa chini ya kifungu cha 30 na ataruhusu afisa aliyekamata kugonga lakiri katika vifaa hivyo au kuchukua sampuli kutoka hapo na sampuli zote zitagongwa lakiri ya afisa huyo na kusubiri amri za hakimu. (2) Afisa ambaye atashindwa kutii masharti chini ya kifungu kidogo cha (1) au akipotea, atatenda kosa na akihukumiwa atatakiwa kulipa faini ya shilingi milioni moja au kifungo cha muda wa miaka mitano. 38. Maafisa wote katika idara mbalimbali zilizotajwa chini ya sheria hii, watatakiwa baada ya kupewa notisi au ombi kufanywa kushirikiana katika kutekekeleza masharti ya sheria hii 39. Pale mtu yeyote anapokamata au kushikilia chini ya sheria hii atatakiwa katika saa arobaini na nane aripoti kuhusu taarifa za ukamataji na ushikiliaji huo kwa mkuu wake wa kazi. Adhabu ya kuingia kwa upekuzi kwa nia mbayaau ukamataji na ushikiaji, 40.-(1) Afisa yeyote amabaye ameruhusiwa chini ya sheria hii kufanya lolote- (a) bila ya sababu za msingi za kuwa na wasiwasi, anaingia au anatafuta au anasababisha kuingia au kutafuta kwenye jengo lolote au mahali; au (b) kwa nia mbaya na bila umuhimu anakamata mali ya mtu yeyote kwa kujifanya kuwa anakamata au anatafuta madawa au vitu vyovyote vya kulevya au kitu kingine, kinachotakiwa kutaifishwa chini ya sheria hii au anakamata nyaraka yoyote au kitu kinachotakiwa kukamatwa chini ya sheria hii; au (c) kwa nia mbaya na bila umuhimu anamfungia, anafanya upekuzi au anamkamata mtu yeyote, anatenda kosa na akihukumiwa atatakiwa kulipa faini isiyozidi shilingi milioni tano au kifungo cha muda wa miezi sita. (2) Mtu yeyote mwenye nia mbaya na makusudi anatoa taarifa za uongo na kusababisha kukamatwa au upekuzi ufanyike chini ya sheria hii anatenda kosa na akihukumiwa anatakiwa kulipa faini isiyozidi shilingi laki tano au kifungo cha mwaka mmoja au vyote faini na 23

kifungo. Adhabu dhidi ya maafisa wanaokataa kutimiza wajibu au kusaidia watuhumiwa Uwezo wa kutaifisha vitu au vifaa,n.k kuhusiana na kosa 41.-(1) Afisa yeyote mwenye wajibu wowote chini ya sheria- (a) anayekataa kutimiza wajibu wake labda awe na sababu halali ya kufanya hivyo; au (b) anamwangalia mwathirika yeyote au mtu mwingine yeyote amabye ameshtakiwa na (c) kosa chini ya sheria hii; anasaidia kwa kujua au anashiriki katika kwenda kinyume na sheria hii au taratibu au amri iliyotolewa, anatenda kosa na akihukumiwa atatakiwa kulipa faini isiyozidi shilingi laki tano au kifungo cha muda wa miaka miwili. (2) Msemo afisa katika kifungu hiki unajumuisha mtu yeyote aliyeajiriwa katika hospitali au taasisi inayotambuliwa au kusimamiwa na serikali kwa kutoa tiba kwa waathirika. (3) Mahakama haitatambua kosa lolote chini ya kifungu kidogo cha (10) isipokuwa lalamiko la mandishi lililofanywa kuhusu adhabu ya Tume. 42.-(1) Pale kosa lolote chini ya sehemu ya IV limetendwa, dawa au kitu cha kulevya, afyumi mkopi, mmea wa mkoka, mmea wa bangi, vifaa au vyombo kuhusiana na kosa lililotendwa vitatakiwa kutaifishwa. (2) Dawa au kitu chochote cha kulevya kilichozalishwa kihalali, kuletwa au kusafirishwa nje ya Jamhuri ya Muungano, kutengenezwa kumilikiwa, kutumiwa, kununuliwa au kuuzwa pamoja na au kwa kuongezea kwa dawa au kitu ambacho kinatakiwa kutaifishwa chini ya kifungu kidogo cha (1) na mifuko yake, vifungashio, vifuniko ambavyo dawa au kitu chochote cha kulevya, vitu, vyombo vinavyotakiwa kutaifishwa chini ya kifungu kidogo cha (1) vinapatikana na vitu vingine vifungashio, vifuniko navyo vitatakiwa kutaifishwa. (3) Mali yoyote iliyotumika kuficha dawa au kitu chochote cha kulevya kinachotakiwa kutaifishwa chini ya sheria hii navyo vitataifishwa pia. 24

(4) Pale dawa au kitu chochote cha kulevya kinapouzwa na mtu huku akijua au akiwa na sababu za kuamini kwamba dawa au kitu hicho kinatakiwa kutaifishwa, pesa zitokanazo na mauzo yake pia yatataifishwa. Utaifishaji kukiwa hakuna kuhukumiwa Dhana ya nyaraka katika kesi fulani 43.- (1) Katika kusikiliza kesi chini ya sheria hii, ama mtuhumiwa amehukumiwa au ameachiwa, mahakama itaamua kama kifaa au kitu kilichokamatwa chini ya sheria hii kitatakiwa kutaifishwa chini ya kifungu hiki na iwapo ikiamua hivyo, itaamuru utaifishaji wake ufanyike ipasavyo. (2) Pale kifaa au kitu chini ya sheria hii kinapoonekana kustahili kutaifishwa lakini aliyefanya kosa hafahamiki au hapatikani, mahakama inaweza kuchunguza na kuamua kuamuru utaifishwaji ipasavyo. (3) Amri ya utaifishaji wa kitu au kifaa haitatolewa- (a) mpaka uishe mwezi mmoja kuanzia siku ile ya kukamatwa; au (b) bila ya kusikilizwa kwa mtu yeyote anayedai (c) haki ;au bila ya ushahidi kama upo uliotolewa kuhusiana na dai. (4) Iwapo kifaa au kitu mbali na dawa au kitu cha kulevya, afyumi mpopi, mmea wa mkoka au mmea wa bangi, kinaweza kuharibika upesi au kwa mtazamo wa mahakama kwamba uuzaji wake utakuwa kwa faida ya mwenye mali, inaweza wakati wowote kuamuru iuzwe, na masharti ya kifungu kidogo hiki yatatumika kwa fedha zilizotokana na mauzo. (5) Mtu yeyote anayedai haki yoyote ya mali ambayo imetaifishwa chini ya sheria hii, anaweza kukata rufaa Mahakama Kuu dhidi ya amri ya utaifishwaji. 44.Ikiwa nyaraka yoyote - (a) (b) imetolewa au kutumwa na mtu yeyote au imekamatwa kutoka kwenye uangalizi au udhibiti wa mtu yeyote chini ya sheria hii,au chini ya sheria yoyote;au imepokelewa kutoka mahali popote nje ya Jamhuri ya Muungano na imekubaliwa na 25

Uwezo wa afisa aliyeruhusiwa kuita taarifa mamlaka au mtu huyo kwa namna kama ilivyoelekezwa na Tume, katika mwenendo wa upepelezi wa kosa lolote chini ya sheria hii, iwapo nyaraka hiyo itatolewa katika mwenendo chini ya sheria hii kama ushahidi dhidi yake au mtu mwingine yeyote ambaye wameshtakiwa naye kwa pamoja, mahakama itatakiwa- (i) kuikubali nyaraka katika ushahidi, bila ya kujali kwamba haijawekwa muhuri ipasavyo, iwapo nyaraka hiyo inakubalika katika ushahidi ; (ii) katika kesi inayoangukia aya ya (a) itachukuliwa kuwa yaliyomo ni kweli pia, labda kama kinyume chake kitathibitika. 45.-(1) Afisa yeyote ambaye ameruhusiwa chini ya sheria hii anaweza,wakati wa uchunguzi unaohusiana na kwenda kinyume na masharti yoyote ya sheria hii- (a) (b) kutaka taarifa kutoka kwa mtu yeyote kwa lengo la kujiridhisha mwenyewe iwapo kuna kwenda kinyume na masharti ya sheria au taratibu au amri iliyofanywa chini yake; kumtaka mtu yeyote kutoa au kupeleka nyaraka yoyote au kitu muhimu au kinachohusiana na uchunguzi. (2) Afisa anayetekeleza madaraka yake chini ya sheria hii au taratibu au amri hatatakiwa kulazimishwa kusema alipata wapi taarifa yoyote kuhusiana na utendaji wa kosa lolote. SEHEMU YA KUKAMATWA KWA MALI ITOKANAYO AU ILIYOTUMIKA KATIKA USAFIRISHAJI HARAMU Ukamataji wa mali Sura ya 256 46.-(1) Kufuatana na sehemu hii, pale mtu yeyote anapohukumiwa kwa kosa chini ya sehemu hii, mali yake wakati wa tarehe ya hukumu au baada ya hapo, itataifishwa na serikali kufuatana na Sheria ya Matunda yatokanayo na Uhalifu. (2) Masharti ya kifungu kidogo cha (1) yatatumika kwa- (a) kila mtu ambaye amehukumiwa kwa kosa chini ya sheria hii; (b) kila mtu ambaye amehukumiwa kwa kosa hilohilo na mahakama yenye mamlaka ya kusikiliza kesi za jinai; 26

(c) kila anayeshirikiana na mtu aliyetajwa chini ya aya za (a) na (b). (3) Kwa madhumuni ya sehemu hii, labda muktadha uhitaji vinginevyo, ushirika maana yake ni - (a) mtu yeyote ambaye amekuwa akisimamia masuala au kuweka mahesabu ya mtu huyo; (b) mdhamini wa dhamana pale- (i) dhamana ilianzishwa na mtu huyo; au (ii) thamani ya mali iliyotolewa na mtu huyo kwa wadhamini inafikia si chini ya asilimia ishirini ya thamani ya dhamana hiyo. (4) Pale afisa aliyeruhusiwa kwa mandishi anaona mali yoyote ya mtu huyo imeshikwa kwa niaba yake na mtu mwingine yeyote, afisa huyo ataamuru mtu mwingine huyo apeleke mali hiyo kwa lengo la kuitaifisha Kukataza kushika mali iliyopatikana isivyo halali Sura ya 256 Kamishna kuruhusu upelelezi au upimaji 47.-(1) Mtu hatatakiwa kuwa na mali iliyopatikana isivyo halali ama na yeye mwenyewe au kupitia kwa mtu mwingine kwa niaba yake. (2) Pale mtu yeyote anaposhika mali yoyote iliyopatikana isivyo halali kinyume na kifungu kidogo cha (1), mali hiyo itataifishwa kwa Tume kulingana na sehemu ya IV ya Sheria ya Matunda yatokanayo na Uhalifu. (3) Mali haitataifishwa chini ya sehemu hii ikiwa mali hiyo ilikuwa ya mtu ambaye sheria hii imetumika kabla ya kipindi cha miaka mitatu kutoka tarehe ambayo alishtakiwa kwa kosa linalohusiana na usafirishaji haramu. 48.-(1) Tume inaweza kumruhusu afisa yeyote au kundi la watu kwa amri au kuelekeza afisa huyo akipata taarifa kwamba mtu yeyote ambaye sehemu hii inamhusu ameshtakiwa kwa kosa ama limefanyika ndani ya Jamhuri ya Muungano au nje, aendelee kuchukua hatua zote muhimu za kutafuta na kutambua mali yoyote iliyopatikana isivyo halali. (2) Pale afisa anayefanya upelelezi au uchunguzi chini ya kifungu kidogo cha (1) anapokuwa na sababu za kuamini kwamba mali yoyote inayohusiana na uchunguzi au upelelezi unaofanyika ni mali iliyopotikana isivyo halali na kuna uwezekano wa mali hiyo kufichwa, kuhamishwa au kushughulikiwa kwa namna ambayo itavuruga mwenendo wowote wa kutaifisha mali hiyo chini ya sehemu hii, anaweza kuamuru utaifishwaji wa 27